Kamati ya wahariri
Dr. L. Patt Franciosi, Ph.D - Rais wa Zamani wa Shirikisho la Afya ya Akili Duniani (WFMH)
Daktari. L. Patt Franciosi, Ph.D ndiye Rais wa Zamani wa Shirikisho la Afya ya Akili Duniani (WFMH). (WFMH) limejitolea kukuza kiwango cha juu kabisa kinachowezekana cha afya ya akili katika mataifa yote. Dkt. Franciosi anawakilisha (WFMH) Kamati kuu ya Global Consortium for the Advancement of Promotion and Prevention in Mental Health (Ubia wa Dunia wa Maendeleo na Ukuzaji na Kulinda Afya ya Akili) (GCAPP), na yeye ni Makamu wake wa Rais. Yeye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mpango wa Mkutano wa Dunia ya Nne juu ya Ukuzaji wa Afya ya Akili na Uzuiaji wa Matatizo ya Akili na Tabia.
Dakt. Franciosi hapo awali alishikilia cheo cha Rais wa Shirika la Kitaifa la Amerika la Afya ya AKili (NMHA), ambayo hufanyakazi kuboresha afya ya akili ya Waamerika wote kupitia utetezi, elimu, utafiti na huduma. Kwa kuongezea, Dakt. Franciosi amehudumu kama Mwenyekiti wa National Prevention Coalition, shirika ambalo lina mashirika rafiki 25 ya afya ya akili, pamoja na (WFMH) na NMHA
Dakt. Franciosi amepokea Cheo cha Rais wa Baraza la Taasisi ya Kitaifa ya Ushauri wa Afya ya Akili na hata pia Baraza la Katibu wa Afya na Huduma ya Wanadamu wa Merikani juu ya Matangazo na Uzuiaji wa Magonjwa. Amepokea tunzo kadhaa kwa kazi yake ya kutetea afya ya akili, haswa katika eneo la afya ya akili ya watoto.
Amelia Mustapha - Makamu wa Rais wa European Depressiyon Association (Shirika la Unyogovu Uropa), Mkurugenzi wa Kituo cha Uingereza cha Afya ya Akili
Amelia Mustapha ni Makamu wa Rais wa European Depression Association (Shirika la Unyogovu Uropa) na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Kituo cha Uingereza cha Afya ya Akili. Hapo awali Amelia alikuwa Mkurugenzi wa Kuchangisha Pesa, Matangazo na Mawasiliano wa Depression Alliance (Muungano wa Unyogovu), Ufadhili unaoongoza Uingereza wa watu waliyoathiriwa na unyogovu.
Amelia ni mfanya kampeni mwenye bidii na wakili mstahamilivu. Alipanga kampeni ya Wiki ya Unyogovu wa Kitaifa ya Uingereza kwa miaka mitano na kusimamia kazi za katibu wa Kikundi cha Vyama vyote vya Bunge vya Uingereza vya Unyogovu. Amelia ameandika zaidi ya vitabu 20 juu ya unyogovu kwa umma na hivi karibuni alikaa katika kikundi cha Taasisi ya Taifa la Uingereza la Ubora wa Hospitali ‘Unyogovu kwa Mwongozo wa Hospitali ya Watoto”.
Prof. Pedro Delgado -– Mwenyekiti wa Idara ya Taaluma na tiba ya magonjwa ya Akili katika Shule ya Utabibu, Kituo cha Sayansi ya Afya cha Chuo kikuu cha Texas, San Antonio, Texas, Marekani.
Pedro Delgado, MD, ni Mwenyeketi, Idara ya Taaluma na tiba ya magonjwa ya Akili katika Shule ya Utabibu, Kituo cha Sayansi ya Afya cha Chuo kikuu cha Texas, San Antonio. Pia anatumika kama Mshauri Msaidizi wa Maendeleo ya Kitivo cha shule ya utabibu.
Dakt. Delgado ni daktari mtaalamu ambaye utafiti wake unapendelea biolojia ya neva na madawa ya matatizo ya mhemko na wasiwasi, unyogovu, dhiki na hali zingine za akili. Ameorodheshwa mara kwa mara katika orodha ya Madaktari Wazuri nchini Merikani tangu 1996. Dakt. Delgado Anajulikana sana kwa kazi yake kubwa ya kutumia vipitisha neva katika uchunguzi wa madawa ya unyogovu. Kwa ajili ya kazi yake ya kutafiti biolojia ya unyogovu, alipata tuzo linalosifiwa la Anna Monika la National Institutes of Health (NIH) –utafiti uliodhaminiwa. Anatumika kwenye kamati ya wahakiki wa maandishi, kama mhakiki wa matangazo ya Baraza la Kanada la Utafiti wa Madawa, Idara ya Mambo ya Wazee, na NIH.
Prof. Michael Bauer - Profesa wa Taaluma na tiba ya magonjwa ya akili na Naibu Mkurugenzi katika Idara ya Taaluma na tiba ya magonjwa ya akili na Matibabu ya Saikolojia katika Chuo
kikuu cha Utabibu cha Charité, Berlin, Shule ya Charité Mitte, Ujerumani
Michael Baur, Md, PhD., ni Profesa wa Tiba ya Akili na Kaimu Mkurugenzi katika Idara ya Tiba ya Akili na Taaluma na tiba ya magonjwa ya akili katika Chuo kikuu cha Utabibu cha Charite, Berlin, Shule ya Charite Mitte, Ujerumani. Kwa kuongezea, Yeye ni Mkurugenzi wa Hospitali ya wagonjwa kwa jumla ambao hawalazwi na Hospitali ya ugonjwa wa Bipolar. Na Mkurugenzi wa Mpango wa Kutafiti Matatizo ya Mhemko, pia katika Chuo kikuu cha Utabibu cha Charite, Berlin.
Utaalamu wa utafiti wa Profesa Bauer unajumuisha biolojia ya neva na utabibu wa matatizo ya mhemko kwa kuzingatia matatizo ya bipolar na unyogovu, na uchunguzi wa mfumo wa kikoromeo katika matatizo ya mhemko kwa kutumia mfumo wa neva na teknolojia ya kuangalia utendaji kazi wa bongo (PET). Yeye ni mdadisi mkuu wa kesi kubwa ya kimataifa juu uzuri wa kipimo cha juu cha levothyroxine katika unyogovu unaodhaminiwa na Taasisi ya Utafiti ya Matibabu ya Stanley, Bethseda.
Michael Bauer amechapisha zaidi ya nakala 120 katika jarida zinazohakikiwa na marafiki, vitabu vitano vilivyohakikiwa na sura 40 za kitabu na amepokea sifa na tuzo kadhaa, pamoja na Tuzo la Mdadisi Kijana la Muungano wa Kitaifa wa Utafiti juu ya Kuchanganyikiwa na Unyogovu (NARSAD), tuzo la 2005 la NARSAD la Mdadisi wa Kujitegemea, Elimu ya bure ya Judson Braun ya Utafiti katika Chuo kikuu cha California, Los Angeles, na Elimu ya bure ya Utafiti ya Deutsche Forschungsgemeinschaft.
Dr. Ricardo Colin - – Naibu Mkurugenzi wa Kufunza katika Taasisi ya Kitaifa ya Nyurolojia na Upasuaji wa neva, Wizara ya Afya, Meksiko
Ricardo Colin ni mtaalamu wa tiba na tibamaungo. Yeye ni Mkuu wa Taaluma na tiba ya magonjwa ya akili katika Chuo kikuu cha La Salle, Shule ya Utabibu, Mji wa Meksiko, na Profesa msaidizi wa tiba ya neva katika Chuo kikuu cha Kitaifa cha Meksiko, idara ya Uzamili, Shule ya Utabibu.
HYeye pia ni rais wa Shirika la tiba ya Neva ya Meksiko na hufanya kazi ya kibinafsi nchini Meksiko, haswa kuwatibu wagonja wenye Shida Kubwa ya Unyogovu na Matatizo ya Bipolar.
Utafiti wake unazingatia Tiba ya Kutikisa kupitia stima (ETC) katika matatizo ya neva.
